Aunt Ezekiel katika harakati za kusaka Mtoto,Dubai
Mwigizaji
 nguli katika tasnia ya filamu Bongo, Aunt Ezekiel (pichani) anadaiwa 
kuanza kusaka mtoto ikiwa ni miaka miwili tangu afunge ndoa na Sunday 
Dimonte. 
Kwa
 mujibu wa rafiki wa karibu wa Aunt, siku si nyingi staa huyo atakwenda 
kuweka makazi ya muda kwa mumewe Dubai hadi atakapopata ujauzito.
Akizungumza
 na Amani hivi karibuni, rafiki huyo ambaye aliomba jina lake 
lihifadhiwe kwa kuogopa kusutwa na ‘matarumbeta’, alisema wengi wanadai 
mume wa Aunt yuko jela kwa hiyo ili kuwahakikishia kuwa kitu hicho 
hakipo ameamua aende kuishi Dubai kwa muda hadi atakaponasa ujauzito.
“Kama
 mipango yake itakwenda vizuri, baada ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani 
kupita ataondoka na safari hii atakaa sana Dubai hadi Mungu 
atakapomjalia kupata mimba ndipo atarejea Bongo. Lakini baadaye 
ataondoka tena kwani hata kujifungua amependa akajifungulie Dubai,” alisema rafiki huyo.
Baada
 ya kupata nyepesinyepesi hizo, Amani lilimtafuta Aunt na kufanikiwa 
kukutana naye uso kwa uso alipoulizwa alisema hapendi kuweka hadharani 
mambo yake na mumewe lakini kuhusiana na ishu ya kwenda kuishi Dubai, 
muda si mrefu ataondoka.
“Nadhani
 unajua kuwa mke na mume Mungu akiwajalia afya njema ni muhimu ndoa 
ijibu kwa kupata mtoto, sasa kuhusu kwenda kuishi Dubai ndiyo mipango 
yangu.
“Nataka kuwakomesha wale wanaodai kuwa mume wangu amefungwa! Sitaki kuwajibu kwa maneno, nataka kuwajibu kwa vitendo,” alitamba Aunt.
 
Chanzo: Amani/Gpl
Chanzo: Amani/Gpl
Tupe maoni yako hapo Chini..!!

 
 
 
Comments
Post a Comment