KAHABA WA KITANZANIA MWENYE ROHO NGUMU AJIELEZEA ALIVYOKUWA AKISAMBAZA NGOMA BONGO.
MWANAMKE
 mmoja wa Kitanzania aliyefanya ukabaha kwa miaka 18 katika miji 
mbalimbali ya Tanzania, likiwemo Jiji Kuu la kibiashara la Dar es Salaam
 na mingine ya Namibia, ameibuka na kueleza jinsi alivyotenda dhambi ya 
kusambaza Ukimwi kwa wanaume wakware.
Licha
 ya kukiri kufanya hivyo, akisema kwa siku alipanga hadi wanaume 
watano,tena bila ya kutumia kinga akisema alidhamiria kuusambaza ugonjwa
 huo hatari alioambukizwa akiwa katika shughuli za ukahaba.
Alijigundua
 ameathirika mwaka 2006. Hata hivyo, katika maelezo yake ameelezea 
kuijutia dhamira yake hiyo, akisema alisambaza kutokana na hasira 
aliyokuwa nayo dhidi ya mwanamume aliyemwambukiza.
“Nilimchukia
 sana kila mwanamume, yeyote aliyejiita mwanamume…nilishindwa tu 
kuwawinda na kuwaua, lakini dhamira yangu ilikuwa kutumia silaha yoyote 
kuua wanaume kwa sababu mmoja wao aliniua… 
“Ndani
 mwangu nilijisemea kamwe sitawaambia hali ya afya yangu, yeyote 
anayekuja kwangu nammaliza. Kwa namna walivyoniambukiza lazima 
niwaambukize’. 
“Sijui nimewaambukiza wanaume wangapi, lakini ni maelfu,” alisema mwanamke huyo ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 32, alipotoa ushuhuda wake kanisani nchini Nigeria hivi karibuni.

 
 
 
Comments
Post a Comment