Mbunge wa KIGOMA Kusini, ni ukweli mtupu huo!.
                             Login 
                               
            
WAKATI Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), 
David Kafulila,  akifunguliwa kesi namba 131/2014 na Kampuni ya 
kuzalisha Umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) na wenzake 
wawili, kwa madai ya kutoa tuhuma za wizi wa tsh Bilioni 200 kutoka 
kwenye akaounti ya Escrow iliyofunguliwa na Serikali kwa ajiri ya 
kutunza fedha za kuilipa IPTL kwa kuzalisha umeme wa dharura.
|  | 
 Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila, akihutubia mkutano wa hadhara.Pesa
 hizo ambazio zilikuwa Bank Kuu ya Tanzania (BOT) zilichotwa na wajanja 
kabla ya kesi hiyo kufunguliwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es 
Salaam, Kesi hiyo inaungwa mkono na Kampuni ya Pan African Power 
Solution Limited (PAP), ikiongozwa na Mwenyekiti wa Kampuni hiyo 
Barbinder Sigh Seth.
Hata hivyo Mbunge huyo amesema hajapata taarifa rasmi za 
kufunguliwa kesi ya madai ya Sh. bilioni 310 mahakamani, na kwamba 
wanaruhusiwa kufanya hivyo kwakuwa wana haki kisheria pamoja na kwamba 
wao ndiyo wezi wa pesa hizo.
Kafulila ametoa kauli hiyo katika kipindi ambacho Chama Chake
 kimeanza ziara ya nchi nzima ikiwa na ujumbe wa 'Bring back our money' 
rudisha pesa zetu ikiwa ni kuishawishi serikali kusimamia wizi huo ili 
pesa hizo ziweze kurudishwa kwa wananchi badala ya kutafunwa na wajanja 
wachache wakati zinatokana na kodi za wananchi.
Mbali na NCCR- Mageuzi kumfukuza Mbunge huyo na kumvua 
uanachama kabla ya kurudishwa Bungeni kwa amri ya Mahakama, kama ilivyo 
kwa  Mbunge wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema,pamoja Hamad 
Rashd wa CUF walivyo fukuzwa, lakini wakarudishwa Bungeni kwa nguvu ya 
Mahakama.
katika suala hili Kafulila na Chama chake hicho cha zamani wameendelea kushirikiana na kuwa pamoja katika suala hilo.
 
 
 
Comments
Post a Comment