SHILOLE NA MZIWANDA NDANI YA SHELA HIVI KARIBUNI,...WANAFIKI KIMYA!.
|  | 
| SHILOLE | 
Msanii 
 wa  maigizo  na  muziki  wa  kizazi  cha  leo, Zena  Mohammed  
'Shilole'  amekuja  juu  na  kusema  anashangazwa  na  habari  
zilizozagaa  mjini  kuwa  yeye  amekataliwa  ukweni....
Akiongea  na  Mpekuzi, Shilole  amesema: "Nashangaa 
 watu  wanasema  eti  nimekataliwa  ukweni  kisa  umri  wangu  kuwa  
mkubwa  kuliko  wa  mwanaume. Ninachokijua  mimi  umri  haujalishi  
katika  mapenzi, kikubwa  ni  upendo  wa  kweli  na  kuheshimiana.
"Habari 
 za  mimi  kukataliwa  ukweni  hazina  ukweli  wowote, na  wala  hakuna 
 mtu  niliyezungumza  naye  kuhusiana  na  hilo  swala  na  wala  
hakuna  ndugu  yeyote  wa  Nuh Mziwanda  aliyeonysha  kutonipenda. 
"Nilipokelewa 
 kwa  furaha  sana  Ukweni  na  habari  njema  ni  kwamba  hivi  
karibuni  mtarajie  kuona  ndoa  ili  wanafiki  tuwafunge  midomo  
yao,"  alisema  Shilole.

 
 
 
Comments
Post a Comment