BAADA YA POLISI KUMRUBUNI MWANAFUNZI WA KIKE WA MJINI MOSHI NINI KINAENDELEA?.
Ashitakiwa kijeshi.
Taarifa kutoka mjini Moshi mkoani Kilimanjaro, zinaarifu kuwa jeshi la polisi nchini limemkamata na kumfikisha katika mahakama ya kijeshi askari wake Pc.Godlisen anayetuhumiwa kumtumikisha katika vitendo vya ngono mwanafunzi wa kidato cha tatu wa shule ya sekondari Okaoni iliyopo wilaya ya Moshi.
Habari
 zinasema kuwa, askari huyo ambaye Septemba 21 mwaka huu alimfungia 
kwenye nyumba ya kulala wageni mjini moshi mwanafunzi huyo na baadaye 
wawili hao kupata ajali mbaya ya pikipiki wakijaribu  kutoroka, aliumia 
kwenye moja ya bega lake na hivyo kushindwa kupelekwa kwenye mahakama ya
 kijeshi.
Kaimu
 kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro, Koka Moita, pamoja na kukiri 
kuwa wameanzisha uchunguzi kuhusiana na tuhuma hizo, alikataa kuweka 
wazi kama askari huyo amefunguliwa mashitaka ya kijeshi.
Kamanda
 Koka aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa, jeshi la polisi 
linafanya uchunguzi juu ya tuhuma hizo na kwamba kama itabainika, askari
 huyo atachukuliwa hatua za kinidhamu kabla ya hatua zaidi kuchukuliwa.
Pamoja
 na jeshi hilo kumfungulia mashitaka ya kijeshi askari huyo, taarifa 
kutoka kwa mmoja wa wazazi wa mwanafunzi huyo zinadai kuwa, kuna juhudi 
za makusudi zinafanywa na askari wa jeshi hilo kutaka kukwamisha 
mashitaka ya kijeshi dhidi ya askari huyo.
Taarifa
 zinadai kuwa, polisi wa kituo kikuu cha polisi mjini Moshi, wanajenga 
ushawishi kwa wazazi wa mwanafunzi huyo kutaka kulimaliza suala hilo 
kienyeji.
Mambobomba inalaani jambo hili; atua kali zitolewa kwa wafanyakazi na wanafunzi wenye tabia za kishetani kama hizi.poleni sana wazazi wa mwanafunzi husika ni kwa kiasi gani mmepambana mpaka mtoto wenu kufikia leo. 


 
 
 
Comments
Post a Comment