Mwanamuziki
wa kizazi kipya, Ommy Dimpoz (kushoto) akizungumza na Ofisa Uhusiano wa
Airtel Tanzania, Jackson Mmbando (katikati) huku mdada flani kutoka
Airtel akiwasikiliza.
Kundi la Wakali Dancers likinogesha katika uzinduzi huo.
Msanii wa filamu za Kibongo, Irene Paul, akifurahia burudani zilizokuwa zikiendelea.
Ommy Dimpoz akibadilishana mawazo na mwanamuziki mwenzake wa kizazi kipya, AY.
Meneja Masoko wa Airtel, akielezea mchakato wa shindano hilo utakavyofanyika.
Ommy Dimpoz akikamua.
Mshereheshaji
katika hafla hiyo, Ephrahim Kibonde, (kushoto) akionesha headphones
baada ya kutangaza shindano la kuimba kwa waliohudhuria hafla hiyo ya
uzinduzi. Kulia ni wadada warembo waliokuwa wakiwahudumia wageni
waalikwa.
Mwandishi Mwani Nyangasa akiimba wimbo wa Christian Bella uitwao “Nani kama mama”.
Jamaa maarufu kwa jina la Moko Biashara akiimba kuwania zawadi ya headphones.
Mdada huyu raia wa Kenya nae akionesha ushindani kuwania simu hiyo.
Irene Paul nae akitupa karata yake.
Majaji ya mpambano huo, Lady Jaydee na AY wakifutilia kiumakini kila mmoja anavyoimba.
Mwisho wa yote Moko Biashara ndiye aliyeibuka mshindi na kukabidhiwa zawadi ya headphones.
KAMPUNI ya Simu za mkononi ya Airtel, juzi, Ijumaa ilizindua shindano
liitwalo Airtel TRACE ambapo mtumiaji wa mtandao wa Airtel atatakiwa
kupiga namba
0901002233 na kuimba nyimbo zake kupitia kwenye simu yake ambazo zitasikilizwa na majaji.
Akizungumza kwenye uzinduzi huo uliofanyika ukumbi wa High Spirit,
uliopo Jengo la IT Plaza, Posta jijini Dar, Meneja Masoko wa Airtel
Tanzania, Aneth Muga, alisema mshindi atakayepatikana hapa nchini
atakwenda kushindanishwa na washindi wengine kutoka nchini 13 za Afrika
ili kumpata mwimbaji bora wa Afrika.
Mshindi atakayepatikana barani Afrika atakwenda kuungana na msanii nyota wa Marekani Akon na kupiga nae kazi.
Comments
Post a Comment