MASHINDANO YA UMISS YARUHUSIWA MAHAKAMANI NCHINI TANZANIA
MAHAKAMA
 ya Hakimu Mkazi Kisutu,jijini Dar es Salaam, jana iliamuru mashindano 
ya urembo Tanzania yaliyopangwa kufanyika Oktoba 11, mwaka huu kuendelea
 baada ya kutupilia mbali maombi ya dharura yaliyowasilishwa na Prashant
 Patel dhidi ya Hashimu Lundenga ya kuzuia kuendelea kuendesha 
kinyang’anyiro hicho kwa madai ya kukiuka mkataba wa makubaliano yao.
  
Kadhalika
 mahakama hiyo imesema maombi ya hati ya dharura yaliyowasilishwa na 
Patel hayana mashiko ya kisheria na kwamba kuzuia kufanyika mashindano 
hayo ambayo wadhamini mbalimbali wamewekeza fedha zao itasababisha 
mgongano wa kimaslahi.
  
Uamuzi
 huo ulitolewa jana na Hakimu Mkazi Frank Moshi  baada ya kusikiliza 
hoja za mawakili wa pande zote mbili kuhusu maombi hayo ya dharura ya 
kuzuia mashindano hayo kufanyika Oktoba 11, mwaka huu.
  
Hakimu
 Moshi alisema mlalamikaji amefungua kesi mahakamani hapo pamoja na 
maombi ya hati ya dharura akiitaka mahakama yake kuzuia mashindano 
kufanyika kutokana na mlalamikiwa kuvunja haki dhidi ya mwanzilishi 
mwenzake Patel.
Alisema
 Patel kupitia hoja za maombi yake, amedai kuwa Lundenga alivunja 
mkataba huo kwa kufanya mawasiliano moja kwa moja na mawakala bila 
kumshirikisha.
  
Hata
 hivyo, mahakama bila kuacha shaka imeona hakuna sababu za msingi katika
 hati hiyo ya kusababisha mashindano hayo yasifanyike na kwamba hayawezi
 kuathiri kesi ya msingi iliyofunguliwa na mlalamikaji huyo.
  
“Mahakama
 imeona hakuna sababu ya kuzuia mashindano hayo kwa sababu wadhamini na 
washiriki wametumia gharama zao na kwamba kwa kufanya hivyo 
kutasababisha mgongano wa kimaslahi” alisema Hakimu Moshi wakati 
akitupilia mbali hati hiyo ya dharula.
  
Akifafanua
 zaidi alisema hati ya dharura ya mlalamikaji haina mashiko kisheria kwa
 sababu kesi yake ya msingi ipo mahakamani na kwamba haina uhusiano na 
mashindano yatakayofanyika Oktoba 11, mwaka huu.
  
Mapema juzi, mahakama hiyo ilitupilia mbali pingamizi la awali la Lundenga lili

 
 
 
Comments
Post a Comment