EBOLA;KINGA YA EBOLA YAANZA MAJARIBIO HUENDA IKAWA SULUISHI.
        Shirika
 la afya duniani leo linaongoza mkutano wa kamati yake ya dharura , 
kutathmini hali ya hivi karibuni kuhusiana na mlipuko wa Ebola .
Mkutano
 huo unafanyaika wakati ugonjwa huo ukiendelea kuenea katika nchi tatu 
zilizoathiriwa zaidi na ugonjwa huo Guinea, Sierra Leone na Liberia - 
ingawa Senegal na Nigeria, ambazo zilikuwa na visa vichache zimetangazwa
 kutokuwa na ugonjwa huo.
Ni mara ya tatu sasa kamati ya dharura ya WHO inakutana .Lengo la sasa ni kutathmini juhudi zilizofikiwa za kudhibiti ugonjwa huo na kuuzuia kuenea.
Kamati hiyo itaangalia hatua zilizopo za uchunguzi wa 
mlipuko huo katika mipaka. Je hatua hizo zinafaa, na je yaweke masharti 
kamili ya kusafiri kwenye maeneo hayo ?
Kuna baadhi ya sababu 
ndogo za kuwa na matumaini - kwa pamoja Nigeria na Senegal zimeweza 
kuzuia kuenea kwa visa vya Ebola . Na awamu ya kwanza ya kinga za 
majaribio zinazoweza kuaminika zinatarajiwa kuwasili Geneva hii leo .
Lakini kinga kamili zilizoidhinishwa dhidi ya Ebola huenda zikapatikana miezi kadhaa ama baada ya mwaka
 
 
 
Comments
Post a Comment