WAZIRI MKUU MH.MAZENGO PINDA AMEHITIMISHA ZIARA YAKE LEO.
Waziri
 Mkuu, Mizengo Pinda akiagana na baadhi ya viongozi wa chama cha Walimu 
Tanzania kwenye uwanja wa ndege wa Bukoba baada ya kuhutubia katika 
sherehe za siku ya walimu duniani zilizofanyika kitaifa kwenye uwanja wa
 Kaitaba mjini Bukoba Oktoba 5, 2014.
Waziri
 Mkuu, Mizengo Pinda akiagana na Mbunge wa Bukoba Mjini, Hamisi 
Kagasheki kwenye uwanja wa ndege wa Bukoba kabla ya kuondoka kuelekea 
Dodoma Oktoba 5, 2014. Mheshimiwa Pinda alikwenda Bukoba kumwakilisha 
Rais Jakaya Kikwete katika sherehe za siku ya Walimu Duniani 
zilizofanyika kitaifa kwenye uwanja wa Kaitaba.

Waziri
 Mkuu, Mizengo Pinda akitazama ngoma ya Kihaya kabla ya kuondoka kwenye 
uwanja wa ndege wa Bukoba Oktoba 5, 2014 ambako alikuwa mgeni rasmi 
kwenye sherehe za siku ya walimu duniani zilizofanyika kitaifa kwenye 
uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba Oktoba 5, 2014. Wengine kutoka kushoto ni
 Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali
 za Mitaa na Mbunge wa Luangwa, Kassim Majaliwa na Mkuu wa Mkoa wa 
Kagera, Kanali Mstaafu, Fabiana Massawe.
Waziri
 Mkuu, Mizengo Pinda akiongozana na Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali 
Mstaafu , Fabian Massawe (kushoto kwake) na Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa
 Kagera, Costansia Buhiya (kulia kwake) kuvuka uwanja wa ndege wa Bukoba
 baada ya kutua kwenye uwanja huo, Oktoba 4, 2014 ambako Oktoba 5,2014 
alikuwa mgeni rasmi kwenye sherehe za siku ya walimu duniani 
zilizofanyika kwenye uwanja wa Kaitaba.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)



 
 
 
Comments
Post a Comment