T.I NDANI YA TANZANIA.
 Rappa
 kutoka nchini Marekani, Clifford Joseph Harris,'T.I' ni mmoja wa 
wanamuziki watakaopiga shoo katika Usiku wa Fiesta 2014 viwanja vya 
Leaders Club.
Rappa
 kutoka nchini Marekani, Clifford Joseph Harris,'T.I' ni mmoja wa 
wanamuziki watakaopiga shoo katika Usiku wa Fiesta 2014 viwanja vya 
Leaders Club.   Ndugu
 Jason Geter, Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Grand Hustle Records ya 
Atlanta, ambayo ndiyo lebo ya T.I pamoja na Mwana Hip-Hop, B.O.B na 
mwingine anayekuja juu maarufu kama Iggy Azalea, atakuwepo katika 
uzinduzi huo utakaofanyika jijini Dar es Salaam ambao umedhihirisha ni 
jinsi gani tukio hili lilivyo muhimu kwa kampuni ya Grand Hustle.
Ndugu
 Jason Geter, Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Grand Hustle Records ya 
Atlanta, ambayo ndiyo lebo ya T.I pamoja na Mwana Hip-Hop, B.O.B na 
mwingine anayekuja juu maarufu kama Iggy Azalea, atakuwepo katika 
uzinduzi huo utakaofanyika jijini Dar es Salaam ambao umedhihirisha ni 
jinsi gani tukio hili lilivyo muhimu kwa kampuni ya Grand Hustle.“Kwa upande wetu, tumefurahi kuleta bidhaa zetu katika bara la Afrika haswa hapa nchini Tanzania, tunadhani hili ni soko kubwa na ambalo lipo tayari kwa bidhaa zetu. Sikuja kuzijulisha bidhaa zetu hapa Tanzania pekee bali pia kuangalia mitindo mbalimbali iliyopo hapa nchini,” alisema Geter.
Duka la Pop Up litafunguliwa kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 9 alasiri na wateja watapata nafasi ya kununua nguo halisi za Hustle Gang, Akoo na Strivers Row, wamiliki wa maduka ya kisasa ya nguo boutique pia wataona bidhaa kwa ukaribu na kutoa oda zao na mashabiki watanunua na tiketi za Serengeti Fiesta hapohapo.
Ziara ya Serengeti Fiesta inatambulika kama tamasha kubwa la muziki na lenye mafanikio katika ukanda wa Afrika mashariki na kati ambalo limeweza kuwavutia zaidi ya mashabiki 500,000 katika matamasha yake yaliyohusisha wanamuziki wa kimataifa kama Jay-Z, Ludacris, 50 Cent, Rick Ross na wengine wengi.
Shoo ya mwisho ya mwaka huu ya tamasha la Serengeti Fiesta itafanyika leo Jumamosi, Oktoba 18, katika Viwanja vya Leaders Club.
 
 
 
Comments
Post a Comment