15 kuuawa katika shambulio Ukraine

Pande zote zinazohusika katika mgogoro wa Ukraine zinatumia makombora yaliyotengenezwa Urusi
Imedaiwa kuwa hakuna 
aliyenusurika katika shambulio la msafara wa wakimbizi katika mji wa 
Luhansk eneo lililo mashariki mwa Ukraine Jumatatu, taarifa ya waasi 
imeiambia BBC.
Taarifa za shambulio hilo bado hazijawekwa wazi 
lakini msemaji wa jeshi la Ukraine amesema miili ya watu 15 imepatikana 
kutokana eneo la tukio.
Ukraine imewashutumu waasi 
wanaoungwa mkono na Urusi kwa kuushambulia msafara wa wakimbizi lakini 
wamekana kuhusika na shambulio hilo.
Wakati huo huo, mapigano makali yameripotiwa katikati ya mji wa Luhansk.
Serikali ya Ukraine imesema Jumamne kuwa 
mapigano ya mtaani yalikuwa yakiendelea na afisa katika wizara ya mambo 
ya ndani ameliambia shirika la habari la Ukraine, Interfax kuwa jeshi 
limekuwa likikomboa mji "Kipande kwa kipande".

Zaidi ya watu 300,000 wamekimbia mapigano mashariki mwa Ukraine
Imeripotiwa kuwa katikati ya mji wa Luhansk kumekuwa na mashambulio ya risasi usiku wa Jumatatu.
Maelfu ya watu wameukimbia mji wa Luhansk, mmoja
 kati ya miji mikubwa miwili inayoshikiliwa na waasi wanaoungwa mkono na
 Urusi, wakati ambapo majeshi ya serikali ya Ukraine yanasonga mbele 
kuikomboa miji hiyo.
Mapigano pia yamekwamisha juhudi za kutafuta 
miili ya watu katika eneo la tukio kufuatia shambulio la Jumatatu usiku,
 katika barabara kati ya ya miji ya Novosvitlivka na Khryashchuvatye.
Zaidi ya watu 300,000 wamekimbia mapigano mashariki mwa Ukraine
 
 
 
Comments
Post a Comment