WAZIRI MKUU WA ZAMANI WA TANZANIA ASHAURI BUNGE LA KATIBA LIHAIRISHWE.
Waziri
 mkuu wa zamani nchini Tanzania Fredrick Sumaye amependekeza kusitishwa 
kwa mjadala wa katiba mpya unaoendelea mjini Dodoma kwa kuwa inaonekana 
dhahiri kuwa si muda muafaka wa kupata katiba mpya kwa sasa.
Amesema
 kusitishwa kwa mjadala huo kutatoa fursa kwa watanzania kujipa muda 
zaidi wa kutafakari ili kufanikisha upatikanaji wa katiba muafaka kwa 
wakati unaofaa.
Kauli
 hiyo ya waziri mkuu wa zamani imekuja wakati bunge hilo linaendelea na 
vikao vyake mjini Dodoma vinavyohudhuriwa na wajumbe wengi kutoka chama 
cha Mapinduzi CCM.
Wakati
 huo huo Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), umesema Rais Kikwete ndiye
 anayeweza kulitolea ufafanuzi suala la kusitisha Bunge Maalum la Katiba
 na siyo mtu mwingine.
Umoja
 huo pia umeendelea na msimamo wa kumtaka Rais kuwasiliana na Mwenyekiti
 wa Bunge hilo, Samuel Sitta kulisitisha  bunge  hilo. 

 
 
 
Comments
Post a Comment