WAGONJWA WA EBOLA WAKIMBIA ZAHANATI

Kituo kilichotengwa na kuwekewa 
karantini kwa sababu ya ebola, kimeshambuliwa na zana kuporwa katika mji
 mkuu wa Liberia, Monrovia.
Watu kama 20 hadi 30 waliowekwa hapo kuangaliwa 
kama wana dalili za ebola walitoroka baada ya kituo hicho kuporwa 
Jumamosi usiku..Mwandishi wa BBC katika kanda hiyo anasema pengine washambuliaji walikerwa kuwa kituo hicho kimewekwa katika mtaa wao.
Wakuu wa Liberia wanajaribu kuwatafuta wagonjwa waliotoroka ili kuwarejesha tena kwenye kituo hicho.
Watu zaidi ya 400 wamekufa kwa sababu ya ebola nchini Liberia kati ya zaidi ya 1,000 katika kanda ya Afrika Magharibi.
 
 
 
Comments
Post a Comment