CHADEMA YAANDAMANA JIJINI DAR-ES-LAAM KUMSHINIKIZA RAIS KIKWETE AVUNJE BUNGE LA KATIBA

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mkoa wa Dar es Salaam, jana kimetoa tamko la kufanya maandamano ili kumshinikiza Rais Jakaya Kikwete, alivunje Bunge Maalumu la Katiba.
 
Pia chama hicho kinatarajia kutoa tamko juu ya kauli aliyoitoa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema juu ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA).
 
Tamko hilo limetolewa na Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi Mkoa Bw. John Mnyika ambaye ni mbunge wa Ubungo, kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Viwanja vya Hananasifu.
 
Awali akizungumza na waandishi wa habari, Katibu Mkuu wa CHADEMA mkoani humo, Enry Kilewo, alisema tamko hilo ni azimio ambalo lilifikiwa kwenye kikao cha baraza hilo mkoa.
chadema
 
Alisema uongozi wa chama hicho mkoa, umetangaza rasmi kuanza mchakato wa kuwania nafasi za uongozi mkoa.
 
Alisema awali Baraza la Wazee lilikaa hivi karibuni na kupokea taarifa za mikoa ya uchaguzi ambayo ni Kinondoni, Ilala na Temeke ambapo katika Mkoa wa Kinondoni, wilaya za uchaguzi za Ubungo na Kawe zilionekana kuwa na matatizo kwenye nafasi ya Mwenyekiti baada ya wagombea wote kutofikia kura asilimia 51.
 
Aliongeza kuwa, baada ya kupokea taarifa hizo uchaguzi huo sasa utarudiwa Agosti 23, mwaka huu ambapo katika Wilaya ya Kawe, Powery Mfinanga alichaguliwa kuwa Mwenyekiti baada ya kupata kura asilimia 62 na kumshinda mpinzani wake Remy Mbidu aliyetepata asilimia 37.6.
 
“Kutokana na chaguzi ndani ya Mkoa kukamilika kwa asilimia 99, Katiba inaturuhusu kuitisha uchaguzi wa Mkoa…fomu za kugombea nafasi mbalimbali zimeanza kutolewa Agosti 17, mwaka huu, mwisho wa kurudisha ni Agosti 20, mwaka huu, saa 10:30 jioni na uchaguzi ukitarajiwa kufanyika Agosti 24, mwaka huu,” alisema.
 
Alisema fomu za uchaguzi zinapatikana katika ofisi zote za chama katika mkoa huo lakini wakati wa kurudishwa, zinatakiwa kurudishwa kwenye ofisi ya mkoa iliyoko Mwananyamala na baada ya hapo zitapelekwa ngazi ya Taifa ili kufanyiwa usaili kwa kushirikiana na uongozi wa kanda.
 
Nafasi zinazogombewa ni Mwenyekiti Mkoa ambayo hivi sasa inashikiliwa na Bw. Mnyika, Katibu Mkuu Mkoa (Kilewo), Mwenyekiti Baraza la Wanawake Mkoa (BAWACHA) inayoshikiliwa na Suzan Lyimo na Katibu wake (Joyce Msuya), ambaye ni Diwani wa Viti Maalumu.
 
Nafasi nyingine ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Mkoa (Hawa Mwaifunga), Katibu wake (Renatus Mlashani), Mwenyekiti Baraza la Wazee Mkoa (Erasto Sibila), Katibu wake nafasi iko wazi.
 
Hivi karibuni viongozi wa vyama vinavyounda UKAWA, walimtaka Rais Kikwete alisitishe Bunge la Katiba na kudai kama halitasitishwa wataitisha maandamano makubwa nchi nzima.

Comments

Popular posts from this blog

STYLE KALI:TUMIA HII NDANI YA DAKIKA MOJA TU MWANAMKE AMEKOJOA.

KISIMI (kinembe) kikichezewa mwanamke anaweza kuwataja maawara zake wote.